NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA BUSEGA

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega amepokea kibali chaajira mpya  kwa barua ya tarehe 7 Desemba 2017 yenye Kumbu Na. FA. 170/533/01/38 kutoka kwa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Raisi Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora  kwa hiyo anawatangazia wananchi wote wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi 14 za kazi kwa kada mbali mbali kama zilivyoorodheshwa hapo chini
 
KATIBU MAHSUSI DARAJA LA III NAFASI 2 TGS B
 
SIFA ZA MUOMBAJI;
Wenye elimu ya kidato cha nne (IV), waliomaliza mafunzo ya uhazili na kufaulu mtihani wa Hatua ya Tatu. Wawe wamefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza maneno 80kwa dakika moja na wawe wamepata mafunzo ya Kompyuta kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali na kupata cheti katika Programu za Windows, Microsoft Office, Internet, E-mail na Publisher.
 
KAZI MAJUKUMU YA KUFANVA
i.    Kuchapa barua, taarifa na nyarakaza kawaida
ii.    Kusaidia kupokea wageni na kuwasaili shida zao, na kuwaelekeza sehemu wanayoweza kushughulikiwa.
iii.    Kusaidia kutunza kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za Mkuu wake na ratiba ya kazi zingine zilizopangwa kutekelezwa katika ofisi anamofanyia kazi, na kumuarifu Mkuu wake kwa wakati unaohitaji   
iv.    Kusaidia kutafuta na kumpatia mkuu wake majalada, nyaraka au kitu chochote kinachohitajika katika shughuli za kazi hapo ofisini.
v. Kusaidia kufikisha maelekezo ya Mkuu wake w akazi kwa wasidizi wake na pia kumuarifu kuhusu taarifa zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi hao.
vi.    Kusaidia kupokea majalada, kuyagawa kwa Maofisa waliokatika sehemu alipo, na kuyakusanya, kuyatunza na kuyarudisha sehemu zinazohusika.
vii.    Kutekeleza kazi zozote atakazokuwa amepangiwa na Msimamizi wake wa kazi
 
=============
 
MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI 7 TGS B
 
sifa za jumla
- mwenye elimu ya kidao cha IV au VI aliyehitimu mafunzo ya Astashahada/Cheti katika moja ya fani zifuatazo Utawala , Sheria, Elimu ya jamii usimamizi wa fedha  maendeleo ya jamii na sayansi ya jamii kutoka chuo cha Serikali za mitaa Homboro Dodoma au chochote  kinacho tamblika na serikali
 
KAZI NA MAJUKUMU
- afisa masuuli na mtendaji mkuu wa Serikali ya Kijiji
- atawajibika kwa mtendaji wa kata
- kuandaa taaarifa za utekelezaji wa kazi  katika eneo lake na kuhamasisha wananchi katika kuandaa na kutekeleza mikakati ya  kuondoo njaa, umaskini na  na kuongeza uzalishaji mali
- kukusanya mapato ya Halmashauri ya Wilaya
- kusimamia utungaji wa sheria ndogo za  Kijiji
- kutafsiri na kusimamia era, sheria na taratibu
- kupokea kusikiliza na kutatua mogogoro ya wanancgi
- atawajibika kwa mtendaji kata
- kusimamia ulinzi na usalama wa raia na mali zao
- kuratibu na kusimamia upangaji wa utekelezaji wa mipnago ya maendeleo ya kijiji
- katibu wa mikutano ya kamatai zote za  Halmashauri ya KIJIJI
- KIiongozi mkuu wa vitengo vya kitaalam katika kijiji
- mwenyekiti wa kikao cha wataalam waliopo katika kijiji nk
 
============
 
DEREVA DARAJA LA II – NAFASI 5 TGS B
 
SIFA ZA KUINGILIA
Kuajiriwa mwenye cheti cha  mtihani wa kidato cha 4 au 6 wenye leseni ya daraja c ya uendeshaji pamoja na uzoefu wa kuendesha magari kwa muda usiopungua miaka mitatu bila  ksababisha ajali
 
KAZI ZA KUFANYA
- kuendesha magari ya abiria namaroli
- Kuhakikisha gari na vyombo vyake vipo katika hali nzuri na usafi wakati wote na kufanya Uchunguzi wa gari kabla na baada ya safari ili kugundua ubovu unaohitaji matengenezo.
- Kufanya matengenezo madogomadogo katika gari.
- Kutunza na kuandika daftari la Safari “Log – book” kwa Safari zote.
- kufanya matengenezo madogo madogo katika gari
 
=============
 
MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II – NAFASI 2
 
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa mwenye Elimu ya Kidato cha IV au VI wenye cheti cha utunzaji kumbukumbu kutoka Chuo chochote kinachotambuliwa na serikali
 
KAZI NA MAJUKUMU
Wasaidizi wa kumbukumbu watafanya kazi zifuatazo hapa chini kwa kuzingatia fani walizosomea na kazi wanazofanya ni kama vile uhifadhi wa nyaraka, uhifadhi wa kumbukumbu za afya, ardhi na masjala ya kawaida
 
KAZI ZA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II
i.    Kutafuta kumbukumbu/nyaraka/mafaili yanayohitajiwa na wasomi
ii.    Kudhibiti upokeaji, uandikishaji wa kumbukumbu/nyaraka
iii.    Kuchambua , kuorodhesha na kupanga kumbukumbu/nyaraka katika makundi kulingana na somo husika (classification and boxing) kwa ajili ya matumizi ya ofisi
iv.    Kuweka/kupanga kumbukumbu/nyaraka katika reki (file racks/cabinets) katika masjala/vyumba vya kuhifadhia kumbukumbu
v.    Kuweka kumbukumbu (barua, nyaraka n.k) katika mafaili
vi.    Kushughulikia maombi ya kumbukumbu/nyaraka kutoka Taasisi za Serikali  
 
MAHSRTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI WOTE 
i. mwombaji awe raia wa Tanzania na awena umri usiozidi miaka 45
ii. waombaji waambatanishe nakala za vyeti vya kuzaliwa
iii. maombi yaaambatane na vyeti vya taaluma  vyeti ya elimu , cheti cha kuzaliwa, na picha 2 passport  za rangi za hivi karibuni na iandikwe jina nyuma
iv. picha moja ya passport size ya hvi karibuni
v. hati za matokeo hazitakubaliwa
vi. waombaji aambao ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia katika utumishi wa umma  wasiomba na wanapaswa kuzingatia katika maelezo yalioko katika  waraka Na. cac.45/257/01/d/140 WA TEREHE  30, NOVEMBA 2010
vii. maombi yaandikwe kwa lugha ya kiswahili au kingereza na yatumwe kwa njia ya posta  kabla ya tarehe 01/01/2018 kwa anuani ifuatayo
 
MKURUGENZI MTENDAJI,
HALMASHAURI YA WILAYA ,
S.L.P 157,
BUSEGA.

Related Posts:

0 Comments: