NAFASI 20 ZA KAZI MTENDAJI WA KIJIJI III HALMASHAURI YA WILAYA YA MERU

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru anapenda kuwatangazia Watanzania wote wenye sifa kuomba nafasi za kazi ya Mtendaji wa Kijiji Daraja la III nafasi 20 kwa masharti ya kudumu na Pensheni, Tangazo hili ni baada ya kupata kibali cha ajira mbadala chenye kumb.Na.FA 170/371/01/71 cha tarehe 08 Novemba 2017 toka kwa Katibu Mkuu Ofisi ya
Raisi Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.


MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI 20
KAZI NA MAJUKUMU
- afisa masuuli na mtendaji mkuu wa Serikali ya Kijiji
- atawajibika kwa mtendaji wa kata
- kuandaa taaarifa za utekelezaji wa kazi katika eneo lake na kuhamasisha wananchi katika kuandaa na kutekeleza mikakati ya kuondoo njaa, umaskini na na kuongeza uzalishaji mali
- kukusanya mapato ya Halmashauri ya Wilaya
- kusimamia utungaji wa sheria ndogo za Kijiji
- kutafsiri na kusimamia era, sheria na taratibu
- kupokea kusikiliza na kutatua mogogoro ya wanancgi
- atawajibika kwa mtendaji kata
- kusimamia ulinzi na usalama wa raia na mali zao
- kuratibu na kusimamia upangaji wa utekelezaji wa mipnago ya maendeleo ya kijiji
- katibu wa mikutano ya kamatai zote za Halmashauri ya KIJIJI
- KIiongozi mkuu wa vitengo vya kitaalam katika kijiji
- mwenyekiti wa kikao cha wataalam waliopo katika kijiji nk
SIFA ZA MWOMBAJI
- mwenye elimu ya kidao cha IV au VI aliyehitimu mafunzo ya Astashahada/Cheti katika moja ya fani zifuatazo Utawala , Sheria, Elimu ya jamii usimamizi wa fedha maendeleo ya jamii na sayansi ya jamii kutoka chuo cha Serikali za mitaa Homboro Dodoma au chochote kinacho tamblika na serikali

MSHAHARA
TGS B yaan 390,000/= Kwa mwezi
MAHSRTI YA JUMLA
i. mwombaji awe lazima we raia wa Tanzania
ii. waombaji lazima awe hajawahi kufungwa kwa makosa ya ya jinai
iii. awe hajawai kufukuzwa au kupunguzwa kazi serikalini
iv. maombi ni lazima yaambatanishwe na vivuli vya vyeti vya kuzaliwa , vyeti vya kuhitimu elimu ya sekondari na vyuo vya mafunzo ya taaluma serult slip hazikubaliki
v. maombi ni lazima yaambatanishwe na picha mbili za passport za hivi karibuni
vi. maombi ni lazima yaambatanishwe na wasifu wenye namba za simu, anuani zenye uhakika pamoja na barua pepe
vii. awe na umri wa miaka 18 na usizidi miaka 45
viii. mwombaji awe hajawahi jiriwa serikalina na hajawahi kupata check namba
ix. waombaji wenye vyeti vya kidato cha 4 na cheti cha taaluma ambavyo vimepatikana nje ya nchi wahakikishe vimehakikiwa na baraza la NECTA na NACTE

Aidha mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 03 Januari 2018 saa 9:30 Alasiri, Pia maombi yatumwe kwa anuan zifuatazo


MKURUGENZI MTENDAJI,
HALMASHAURI YA WILAYA YA MERU,
S.L.P 462
USA -RIVER
Tanganzo hili linapatikana kwenye tovuti ya www.merudc.go.tz  na mbao za matangazo

0 Comments: