Mtendaji wa kijiji daraja la III

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Tabora Uyui anawatangazia nafasi za kazi kwa wananchi wote wenye sifa za kuomba nafasi hizo kama

inavyoonyesha hapo chini

MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III - NAFASI 14

SIFA ZA MWOMBAJI

Awe amehitimu elimu ya kidato cha Sita/Nne na Mafunzo ya Astashahada/cheti katika moja ya fani zifuatazo: Utawala, Sheria, Elimu ya Jamii, Usimamizi wa Fedha, Maendeleo ya Jamii na Sayansi ya sanaa kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo Dodoma, au Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.

KAZI ZA KUFANYA

- Afisa Masuuli na Mtendaji Mkuu wa Serikali ya Kijiji.

- Kusimamia ulinzi na Usalama wa raia na mali zao.

- Kuratibu na kusimamia upangaji wa utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya Kijiji.

- Katibu wa Mikutano na Kamati zote za Halmashauri ya Kijiji.

- Kutafsiri na kusimamia Sera, Sheria na Taratibu.

- Kuandaa Taarifa za Utekelezaji wa kazi katika eneo lake na Kuhamasisha wananchi katika kuandaa na kutekeleza mikakati ya kuondoa njaa, umaskini na kuongeza uzalishaji mali.

- Kusimamia, kukusanya na kuhifadhi kumbukumbu zote na Nyaraka za Kijiji.

2.3. MSHAHARA

TGS B1 - Tshs 390, 000/=

UMRI

Mwombaji awe na umri wa kuanzia miaka 18 hadi 40 na awe Raia wa Tanzania

MAELEZO YA JUMLA

- barua ya maombi iambatane na nakala ya vyeti vyake vya elimu ya sekondari na vyuo pamoja na taarifa binafsi

- muombaji abandike picha 2 za passport za hivi karibuni katika buara yake ya maombi

- hakikisha unaweka namaba ya simu na anuani ya posta

maombi yatumwe kwa

Mkurugenzi Mtendaji (W),

Halmashauri ya Wilaya ya Tabora

S.L.P 610,

TABORA.

Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 22 Januari 2018



















Related Posts:

0 Comments: